KUHUSU HUDUMA

 
HUDUMA YA ELISHADAI
 

Dhamira ya huduma hii ni :

Shalom,
Ni huduma ambayo ilianzishwa  mwaka 2008, chini ya wanafunzi wa MOA sekondari ikiongozwa na mwasisi na mbeba maono hayo Mwl. Mrosso AB. 
Katika wakati ule ilifanyika kama ni sehemu ya kukutana wanafunzi wenye kumjua Yesu Kristo ni nani katika maisha yao.
Wakati ulipo zidi ikawa wenye uhitaji na huduma ni wengi na mchanganyiko wa madhehebu na dini  hivyo huduma iliwapokea kwa wingi sana na hasa ilikuwa ni mwishoni mwa  mwaka 2009.
Huduma ilipanuka hata kuenea mbali na kuifanya kila leo kubadilika kutokana na uhitaji wa kiroho hususani katika utendaji wake.
“KUENEZA HABARI YA UFALME WA MUNGU, na kufanya jamii katika ujumla wake kuwa tayari kwa saa ile ijayo ambayo yaja kama mwizi''
 
  •      UONGOZI KAMILI:
  • Mkurugenzi mkuu,
  • Katibu mkuu na msaidizi wake,
  • Mweka hazina mkuu na msaidizi wake.
  • Idara ya Maombi,
  • Idara ya Mawasiliano,
  • Idara ya Jamii.



Kufikia August,4,2016 huduma itaweza kufanya shukran mara kumi katika kituo cha watoto wenye uhitaji.
Tumeanza kuandaa vitabu mbali mbali vyenye kujenga na kueneza injili kwa sasa kitabu kimoja kipo tayari,

''TAMBUA NGUVU ILIYOKATIKA MAAMUZI YAKO JUU YA MAFANIKIO YAKO''







''MILIKI NA UTAWALE KATIKA KRISTO YESU.''
(Yoshua 1:3        Yeremia 1:10)